Friday, July 26, 2013

"NGUVA" Wa Ukweli Avuliwa, Alimbembeleza Muhusika Amtunzie Siri ya Uwepo wake!!!

-->

Jumanne ya wiki hii huko Ibadan Nigeria, Mwanamke anayefahamika kama Ramota, ambaye ni muuzaji wa samaki wabichi ambao huvuliwa nakuwekwa katika mafriji alikutana na mkasa wa aina yake baada kukutana uso kwa uso na Samaki aina ya Nguva katika Moja ya Matenga ya Samaki aliyoyanunua.

Katika Harakati zake za Kuwatoa samaki hao na kuwapanga, Ramota alikutana na Samaki huyo mwenye Umbile na Nusu Mtu, Nusu Samaki, Hapo Mwanamke huyo alipiga kelele za kuomba msaada kwa majirani na akakimbia mbio kutoka nje.

Ramota alikimbia mpaka kwa Shehe mmoja wa maeneo ya Karibu ili aende kumsaidia, kutokana na kelele alizopiga na baada ya dakika chache kuonekana anarudi na Sheikh, watu walianza kujaa eneo la kazi la dada huyo.

Watu wachache walifanikiwa kumwona kiumbe huyo ingawa hawakupenda kuzungumzia zaidi ispokuwa mwanamke mmoja ambaye alikiri kumwona Nguva huyo na kwamba Ramota hakupaswa kupiga kelele wala kujaza watu kwani Samaki Mtu huyo alimwambia Asiseme kuhusu Kuwepo pale na kwamba alikuja kwa ajili ya kumnufaisha yeye.

Imeelezwa ya kwamba samaki mtu huyo alikuwa akiyasema maneno hayo huku akijificha na nywele zake zenye muundo wa rasta, huku akionekana kukamilika viungo vyote vya usoni licha ya udogo aliokuwa nao.

Kutokana na  zengwe la kujaa watu ilimbidi Ramota na Baadhi ya ndugu na Ma sheikh kumchukua Kiumbe huyo na kuondoka nae hapo kuelekea kwa Ndugu yao Mwingine.

Angalia Vizuri Picha aliyopigwa kupitia simu Kiumbe Huyo.



Nguva akimsihi asimtaje

No comments:

Post a Comment

Blogger Widgets