Friday, January 31, 2014

tufanye kazi kwa maendeleo ya taifa letu

BABU MPENDA TOTOZ, AFUMWA UCH** WA MNYAMA NA KADENTI CHA SHULE, GUEST HOUSE.


YELEUUUWI! Ile tabia ya wazee ya kupenda dogodogo imemtokea puani mzee aliyetajwa kwa jina moja la mzee Omari, ni Ijumaa pekee lenye ubavu wa kuripoti sinema hiyo ya bure.
AIBU YA MWAKA: Babu akifunika uso wake baada ya kunaswa na denti gesti.
Mzee huyo alinaswa laivu akiwa gesti na denti wa shule moja ya sekondari jijini Dar (jina la denti na shule vinahifadhiwa kimaadili).
Tukio hilo la aibu lilijiri juzikati kwenye gesti moja iliyopo maeneo ya Kawe, Dar na kusababisha timbwili zito.
TAARIFA MEZANI KWA OFM
Hivi karibuni, kikosi maalum cha Oparesheni Fichua Maovu (OFM) chini ya Global Publishers, kilipokea lalamiko kutoka kwa mzazi wa denti huyo ambaye alieleza juu ya mabadiliko ya mwanaye kitabia na kushuka kitaaluma kutokana na kusumbuliwa na ‘mbaba’ huyo.
Mzazi huyo aliiambia OFM kuwa amekuwa akifuma mawasiliano ya kwenye simu ya mkononi ya mwanaye na mwanaume huyo ambaye alikuwa hamfahamu.
FUNDISHO KWA WAZEE: Babu akijiandaa kuvaa nguo yake ya ndani baada ya kunaswa gesti.
CHANZO
Mama huyo alisema kuwa kutokana na maendeleo ya mwanaye kuzidi kudorora shuleni, aliamua kumfuatilia kwa karibu kwa kuwa hakutaka apotee.
Mama huyo alitiririka kuwa, siku ya tukio, alimsikia mwanaye huyo akiwekeana miadi kwenye simu na mwanaume huyo ndipo akaamua kumuwekea mtego.
Alisema wakati mwanaye huyo akilonga kwenye simu, yeye alibana sehemu na kuyasikia yote ambayo alikuwa akiyaongea na kwamba walipanga kukutana baa.
“Nilichokifanya nilimpigia simu mjomba wake na kumweleza kila kitu, nikamwelekeza namna ya kumfuatilia. Alichukua bodaboda na kuanza kumfuatilia. Mimi na timu yangu tulifuata nyuma,” alisema mama huyo kwa uchungu.
CHINI YA ULINZI: Babu akiwa mikononi mwa wanausalama.
Alisema mzee huyo alikubaliana na mwanaye wakutane kwenye baa hiyo ambapo ndani yake kuna nyumba ya kulala wageni a.k.a gesti.
OFM YAITWA
Baada ya mpango wa mtego kukamilika ndipo mama huyo akawaita OFM ambao huwa hawalazi damu hivyo walifika mara moja.
TAARIFA POLISI
Kabla ya kuchukua hatua yoyote, walishauriana kutoa taarifa kituo cha polisi, jambo ambalo lilifanyika na kupatiwa msaada wa kiusalama.
NI SAWA NA BABU YAKE
Walipofika kwenye baa hiyo mama mtu alipigwa na butwaa kumuona mtu aliyekuwa akiwasiliana na mwanaye ni mzee sawa na babu yake.
“Yaani jamani kweli dunia imekwisha, mwanangu ni sawa na mjukuu wa huyu mzee, ama kweli tamaa mbaya sana,” alisema mama huyo kwa uchungu.
Huku wakifuatiliwa kwa karibu, mzee huyo na denti walipiga madikodiko na vinywaji ndipo wakatimba kwenye gesti hiyo.
Kilichofanyika ni kwamba polisi na mama wa denti walizama gesti hiyo na kuomba kumsaka mwanafunzi huyo, jambo ambalo halikupingwa.
FUMANIZI LAIVU
Baada ya kuzama ndani ndipo mtego ukafyatuka ambapo mzee Omari alibambwa katika moja ya vyumba vya gesti hiyo huku akiwa amejifunga taulo tu.
Mzee huyo alipatwa na taharuki kubwa asijue la kufanya kufuatia timbwili zito alilozua mama wa denti huyo.
“Kha! Kazi kuharibu watoto wa wenzenu, hivi angekuwa wa kwako ukakuta akifanyiwa hivi ungejisikiaje? Nasomesha kwa gharama kubwa wewe unataka kuniharibia. Hivi hujui mtoto anauma?” alihoji mama huyo kwa hasira huku akimtandika mwanaye vibao.
OMBI
Mara baada ya mzee huyo kunaswa, aliomba chondechonde kukaa na familia ya mwanafunzi huyo ili kuyamaliza yasifike mbali.
Hata hivyo, baada ya maombi ya muda mrefu walikubaliana kuandikishiana ambapo mzee huyo alitakiwa kulipa faini.
“Sisi hatuna maneno mengi, hatutaki kesi ila atulipe fidia ya kumsababishia mtoto wetu asiwe na mahudhurio mazuri shuleni kutokana na ulaghai wake,” alisema mzazi huyo.
MZEE AINGIA MITINI
Habari zilieleza kuwa mzee huyo alishindwa kulipa mara moja badala yake aliingia mitini kwa kigezo kuwa anakwenda kutafuta faini hiyo.
Hadi OFM inaondoka eneo la tukio mzee huyo alikuwa hajawasilisha faini waliyokubaliana hivyo tunafuatilia na tutakachobaini tutaandika katika matoleo yajayo.
FUNDISHO
Hivi sasa kumeshamiri tabia ya wazee kupenda kuharibu mabinti wadogo hivyo kunaswa kwa mzee huyo litakuwa fundisho kwa wengine kwani OFM ambao huwa haikosei, imeamua kulivalia njuga suala hilo. Subirini muone!

GPL.

KANYE WEST ALIPA ZAIDI YA MILIONI 350 ZA KITANZANIA KWA YULE DOGO ALIYEMWANGUSHIA KICHAPO BAADA YA KUMSEMEA MBOVU KIM K.


Wiki chache zilizopita, ililipotiwa kuwa Kanye West alimshambulia mvulana wa miaka 18 kwenye sehemu ya mapokezi ya ofisi za chiropractor.

Na sasa kwa mujibu wa TMZ, Kanye amefikia makubaliano nje ya mahakama ili kumalizana na kijana huyo kwa kumlipa fidia ya $250. Familia ya kijana huyo mdogo imesema kwamba hiyo ilistahili kulipwa kwa kitendo alichofanyiwa kijana huyo na Kanye.

DC Blog.

A-Z, KUJINYONGA KWA MSANII WA BONGO MOVIES HII HAPA


SAKATA la kujinyonga kwa msanii wa filamu Bongo, Victor Peter limegubikwa na matukio tofauti ya kustaajabisha ambayo marehemu aliyafanya siku kadhaa kabla hajapatwa na umauti, Ijumaa limefukunyua kila kitu.
Mwili wa marehemu Victor Peter ukipelekwa mochwari.
Kwa mujibu wa rafiki wa marehemu, Hamisi Koba, msanii huyo alijinyonga usiku wa Februari 27, mwaka huu mkoani Tanga ambapo marehemu alifika jijini humo kuigiza filamu yake iitwayo Our Family.
Hamisi alisema Victor aliwasili jijini humo akiwa na timu ya wasanii sita na kufikia kwenye nyumba ya kulala wageni iitwayo Safari Junior iliyopo maeneo ya Kisosora ambapo punde walianza kushuti filamu hiyo ambayo yeye na Mzee Jengua ndiyo walikuwa wahusika wakuu.
Marehemu Victor Peter enzi za uhai wake.
“Mimi ndiye nilikuwa kama mwenyeji wake mkubwa hapa Tanga, alikuwa ni mpole na siku zote tulipokuwa kazini kwa ajili ya kushuti filamu hiyo aliniambia mambo mengi kuonesha amejipanga kuhakikisha anaifikisha mbali.
“Victor alitokea Mwanza, akaenda Dar ambapo alifika na kuandaa filamu yake ya kwanza aliyoiita Chozi ambayo tayari ilikuwa imekamilika na kuiuza kwenye Kampuni ya Kapiko ya jijini humo,” alisema Koba na kuongeza:
“Filamu hiyo ilikuwa bado haijatoka, akaamua kuja Tanga kuandaa filamu hiyo ya pili ambayo nayo ilikamilika juzi. Naumia sana ninapokumbuka mipango yake maana alikuwa ana ndoto za kufanya makubwa.
Wasanii wenzake na marehemu wakilia kwa simanzi.
“Siku ya Januari 27 tulipokuwa tunakamilisha filamu, kuna muda alikuwa anaonekana kama ana wenge hivi... alipomaliza kushuti sehemu yake tulienda benki, akachukua fedha na kuwalipa wasanii wote.”
Akiendelea kutiririka juu ya tukio hilo, Koba alisema marehemu alionesha kama alikiona kifo chake kabla kwani aliuliza mara mbilimbili kama kuna mtu anamdai ili amlipe.
“Wakati anatupatia fedha kila mara alikuwa anauliza kama kuna mtu anamdai hadi tuliingiwa wasiwasi na ingawa wengine walisema atakuwa amefurahia labda kumaliza muvi yake,” alisema.
Koba alizidi kueleza kuwa, marehemu akiwa na furaha ya kumaliza muvi hiyo, alikwenda chumbani kwake na kujifungia lakini alfajiri (Januari 28) walipomgongea mlango waligundua amejinyonga.
Baadhi ya mashuhuda wakiwa eneo la tukio.
“Tulichungulia kupitia tundu la funguo tukaona kama ananing’inia ndipo tukaenda kwenye kituo cha Polisi cha Chumbageni na kuchukua askari ambao walishirikiana na mwenye gesti hiyo kuvunja
mlango na kumkuta kajinyonga, tukachukua mwili na kuupeleka kwenye Hospitali ya Bombo, mipango ya kuusafi risha mwili kwenda Kahama nyumbani kwao imeanza,” alisema Koba na kuongeza:
“Kwenye hiyo filamu yake, stori ilikuwa mzee Jengua kama baba wa Victor ambapo Mzee Jengua alikufa na baadaye Victor anakufa kiajabu, kifo kimempata kweli.”
Kuhusiana na kifo hicho, Koba alisema kilimuuma kwani alikilinganisha na kile kilichomtokea marehemu Steven Kanumba ambaye pia aliigiza filamu ya Power of Love ikionesha anakufa, akafa kikwelikweli.
Mwili wa marehemu uliokuwa umehifadhiwa katika Hospitali ya Bombo ulitarajiwa kusafi rishwa juzi kwenda nyumbani kwao Kahama kuzikwa.

GPL

GURUMO AFAGILIA DIAMOND PLATINUMZ KWA KUWAKAMUA WATOTO WA KIKE TOFAUTI TOFAUTI, ADAI WANAJIPELEKA WENYEWE.


MSANII mkongwe wa muziki wa dansi Bongo, Muhidini Gurumo ambaye kwa sasa amestaafu, amefungukia skendo ya kuwa na mademu wengi inayomuandama Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Akipiga stori na Ijumaa hivi karibuni maeneo ya Ilala jijini Dar, Mzee Gurumo alisema: “Diamond ana nidhamu sana ila vile anavyotamba jukwaani na kudatisha mashabiki hapo ndipo balaa linapokuja, watoto wa kike wenyewe wanaanza kujisogeza kwake.
Mzee Muhidini Gurumo.
“Pamoja na skendo za mademu zinazomuandama, siwezi kumshusha thamani, ana haki ya kujiopolea mwanamke yeyote anayempenda, yeye kama mwanaume rijali wakati mwingine ni vigumu kujizuia na vishawishi hivyo.”
GPL.

WOLPER APAGAWA NA PENZ* LA JAMAA WAKE MPYA, AWACHANA WATU WASIMSHOBOKEE!!


THE Ijumaa Sexiest Girl 2012, Jacqueline Wolper amesema kuwa, ana imani kubwa na mpenzi wake wa sasa aliyemtambulisha kwa jina la G Modo akiamini atampoza machungu aliyoyapata kutoka kwa mpenzi wake wa zamani, Abdallah Mtoro ‘Dallas’ huku akiwatahadharisha mashosti zake kutoleta shobo (kuwa mbali naye).
Jacqueline Wolper.
Akipiga stori na paparazi wetu hivi karibuni, Wolper alisema anafikia hatua ya kusema hayo kwa kuwa muda mfupi aliokuwa naye amegundua ni mwanaume anayejitambua na anayeheshimu mapenzi ila akawataka mashosti zake kutomsogelea.
“Tangu niwe na huyu kijana nimekuwa ni mwenye furaha kubwa, nasahau hata yale machungu niliyopata kwa mpenzi wangu wa zamani. Lakini najua wapo wanaomtolea macho, tusitafutane ubaya, kila mtu na maisha yake,” alisema Wolper.
GPL.

KILA MTU NA "ULEVI" WAKE, JE WAJUA STAREHE YA WASTARA NI NINI?!!!!


MSANII wa filamu, Wastara Juma amefunguka kuwa starehe yake kubwa duniani ni kukumbatiwa na anapofanyiwa kitendo hicho na mtu wa jinsia yoyote huwa hoi.
Wastara Juma.
Akistorisha na paparazi wetu, Wastara alisema: “Mimi napenda sana kukumbatiwa au kukumbatia, awe ni mwanaume au mwanamke, ndugu yangu au hata kama siyo ndugu yangu, tukikumbatiana tu najisikia raha sana.
“Unajua kila mtu anakuwa na kitu anachokipenda duniani sasa mimi starehe yangu ndiyo hiyo hata marafiki zangu wanajua kwamba mimi napenda kukumbatiwa.”

BASATA "WAMVURUGA" SNURA MAJANGA


KATIKA toleo namba 859 la Desemba 29 hadi Januari 2, 2014 la gazeti hili, kwenye safu yetu hiihii, niliandika kuhusu Snura Mushi, msanii anayetingisha anga la muziki wa mduara. Yupo juu kwa kuwa kibao chake cha Majanga kinasumbua mno hivi sasa.
Snura Mushi.
Kwa wale ambao hawakubahatika kunisoma, niliandika nikionyesha masikitiko yangu kwa namna binti huyu anavyocheza akiwa jukwaani na hata kwenye video zake.
Kama haujawahi kumuona akiwa jukwaani, ni kwamba Snura anajua hasa kukichezea kiuno chake, ni mjuzi wa kukizungusha kwa namna ya kuburudisha kabisa na hatari zaidi, pale anapoamua kuwapa mgongo mashabiki walio ukumbini, kisha akawatingishia kwa namna ya kutetemesha makalio yake makubwa!
Ni aina ya uchezaji ambao kwa watu wazima, ni burudani mno, hasa kama wakati huo, tayari wale wa kiburudisho wanakuwa wamepata moja mbili. Uchezaji wake unaleta mfadhaiko zaidi hasa kutokana pia na uvaaji wake. Amechagua kuwa mtu mwenye mavazi tatanishi.
Lakini kama baba au mama waliostaarabika, hawawezi kujisikia vizuri kumuona msichana huyu akiwajibika jukwaani wakiwa na watoto wao, bila kujali kama ni wasichana au wavulana. Ni aibu, kinyume cha maadili na tena, hamna chochote ambacho watoto wadogo wanaweza kujifunza.
Katika habari ile, niliwashauri pia Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), baada ya kuwa wamefanikiwa kupunguza ujinga wa waigizaji wa filamu wavaa nusu utupu, kuanza kukagua pia video za wasanii wa muziki wa kizazi kipya, kwani wapo wengine wanaojaribu kujitoa ufahamu, wakivaa Kimarekani wakati tunajua wazi kwao ni Kilosa.
Ni jambo linalotia faraja kuja kusikia kuwa BASATA, limeipiga marufuku video ya Snura ya wimbo wake mwingine, Nimevurugwa. Sijawahi kuiona video hiyo, lakini kwa namna ninavyomfahamu msanii huyu anavyoshughulika akiwa jukwaani, ni rahisi kuelewa kilichomo unaposikia kuhusu kuzuiliwa kwake.
Nichukue nafasi hii kuipongeza sana Basata, lakini wakati huohuo kutoa wito kwa chombo hicho cha serikali, kuangalia kwa jicho kali zaidi nyimbo nyingine zinazopigwa katika vituo vyetu vya televisheni, kwani wameruhusu ‘uzungu’ usio na maana kwa jamii, kana kwamba watu wanafuata maungo ya wacheza shoo badala ya kusikiliza ujumbe.
Inasikitisha kuona kwamba licha ya uchezaji huo wa kujidhalilisha, bado kuna msanii mwingine naye amemuiga karibu kwa kila kitu. Naye amekuwa akicheza na kuvaa kwa namna inayowadhalilisha sana mama zetu, lakini kwa namna ya kushangaza, wenyewe wamekuwa wakijisikia fahari na kuamini wanavutia.
Nimekuwa nikisema mara kwa mara kwamba wasanii wetu, hasa wale wanaobahatika kuwa nyota kwa kazi zao, wanapaswa kuwa mfano mbele ya jamii. Wanatakiwa wajue kuwa miongoni mwa mashabiki wa kazi zao, ni watoto wadogo, dada, kaka, shangazi na wazazi wanaojiheshimu. Unajaribu kujiuliza, hivi Snura anaweza kukata mauno kwa jinsi ile mbele ya wazazi wake?
Kwa vyovyote jibu la swali hili litakuwa ni hapana, vinginevyo labda awe na matatizo yasiyo ya kawaida kwenye kichwa chake. Sasa kama hawezi kucheza namna ile mbele ya wazazi wake, anajisikiaje anapofanya vile mbele ya wazazi wa wenzake?
Ni kweli biashara ni ubunifu, lakini inapendeza zaidi ubunifu wetu ukazingatia pia maadili yetu kama jamii yenye kuheshimiana. Uchezaji wa Snura jukwaani, unatoa ushawishi mkubwa kwa shabiki anayemsogelea kumshika makalio.
Mimi bado ni shabiki mkubwa wa maadili na ninaamini kutoka moyoni kwamba mashabiki wa muziki wa kizazi kipya wanavutiwa zaidi ya tungo kuliko uvaaji wa nusu uchi jukwaani.
Snura, Shilole na wasanii wengine wanaovaa na kucheza kihasara hasara, wanapaswa kubadilika kwa faida ya watoto wetu ambao utandawazi unaonekana kuwapoteza zaidi badala ya kuwasaidia!
GPL.

Thursday, January 30, 2014

MUIGIZAJI WA MOVIES ZA NG0N0 AMUOTA D'BANJ AKIMPA "MAVITUS" ANGALIA ALICHOANDIKA HAPA KATIKA TWITTER PAGE YAKE.


Yule Muigizaji wa Movies za Ng0n0 wa nchini Nigerioa, Afro Candy ameandika katika ukurasa wake wa Twitter ya kwamba amemuota mwanamuziki D'banj anampa raha za dunia, na jinsi anavyoelewa kwamba jamaa huyo kapendelewa maombile ya kiume anatamani ampate haraka iwezekanavyo ili atulize kiu yake hiyo.

Wednesday, January 29, 2014

HATIMAYE SHILOLE ANASA KWA MCHUMBA WA KIZUNGU.

KWA mara ya kwanza msanii wa filamu na muziki Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amenaswa akiwa na mwanaume wa Kizungu anayedaiwa kuwa ndiye mchumba wake.
Zuwena Mohamed ‘Shilole’ akiwa na mchumba wake.
Chanzo makini kimepenyeza habari kuwa, safari za mara kwa mara za Shilole nchini Uingereza zimekuwa zikisababishwa na mchumba huyo wa Kizungu ambaye huwa anamuita kufurahia p#nzi lao pamoja na kumtafutia shoo mbalimbali.
“Ukweli ni kwamba Shilole ana mchumba wa Kizungu na walikutana kwenye shoo ya mara ya kwanza aliyoenda kufanya nchini Uingereza na hivi karibuni ataenda tena na amealikwa na huyo mchumba wake,” kilisema chanzo hicho.
Gazeti hili limekuwa la kwanza kunasa picha kadhaa za Shilole akiwa katika mapozi tofauti ya kimahaba na Mzungu huyo.
Baada ya chanzo hicho kumwaga ‘upupu’ huo, mapaparazi wetu walimtafuta Shilole ili aweze kufunguka ambapo bila kuumauma maneno, alikiri kuwa amepata mchumba huyo aliyemtambulisha kwa jina la Ankar.
Akizidi kumwaga data za boifrendi wake huyo, Shilole alisema awali walikutana kwenye moja ya shoo zake nchini humo ndipo urafiki ulipoota mizizi na kufikia hatua ya kuwa wap#nzi.
“Kweli nina mchumba Mzungu ambaye ni raia wa Uingereza, nilipokuwa napataka nimefika, sipindui tena. Unajua muziki wangu na mauno yangu yanawavutia sana watu, siku ya kwanza aliniona kwenye shoo akanipenda ndipo tukaanzisha urafiki.



“Hivi karibuni nina safari ya kwenda nchini humo kwa mwaliko maalum alionipa, nitaenda peke yangu kwani safari nyingine zote zilizopita nilikuwa naenda na watu,” alisema Shilole.

MAMA WEMA SEPETU AWASAKA DIAMOND NA MWANAE ILI AWAANZISHIE VARANGATI.

HABARI mpya! Mama wa Miss Tanzania 2006/07, Wema Isaac Sepetu, Mariam Sepetu anadaiwa kuingia rasmi mitaani akiwasaka wap#nzi, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Wema, chanzo cha uhakika kimesema na Amani.
Wema na Diamond wakiwa katika pozi la kim@haba.
Kwa mujibu wa chanzo hicho makini, mama Wema ameamua kuchukua uamuzi huo baada ya kusikia taarifa kutoka kwa watu kwamba, Diamond amekuwa akisambaza maneno mitaani kuwa haogopi vitisho vya mwanamke huyo kufuatia hatua yake ya kumrudia binti yake.
ILIKUWAJE KWANI?
Hivi karibuni, mama Wema alizungumza na gazeti tumbo moja la hili, Ijumaa Wikienda linalotolewa na Kampuni ya Global Publishers Ltd kila siku ya Jumatatu na kusema kitendo cha Diamond kumrudia bintiye hakubaliani nacho.
Aliongeza kuwa, kufuatia hatua hiyo iko siku ataingia mtaani kumsaka Diamond na popote pale atakapomnasa, atamkata na panga.
Mama Wema, Mariam Sepetu anayewasaka wap#nzi hao.
TURUDI KWA CHANZO
“Jamani si mnakumbuka juzikati mama Wema alisema atamsaka Diamond? Sasa amesikia Diamond anatangaza mitaani kwamba, hatishiki na tamko la mama mkwe wake huyo na watakapokutana watajua nani zaidi.
“Hivi ninavyosema, mama Wema ameingia mtaani kuwasaka. Lengo lake awakute wote wawili ili awaanzishie timbwili la kufa mtu.
“Tangu Ijumaa iliyopita, kila siku anatoka kwenda mitaani kuwasaka, naamini siku akiwakuta pamoja kweli itakuwa vita kubwa,” kilisema chanzo chetu.
Gari la Wema na la Diamond yakiwa yameegeshwa nyumbani kwa Wema.
KWA NINI ASIENDE NYUMBANI?
Chanzo kilipoulizwa kama kweli mama Wema amepania kuwanasa wawili hao, kwa nini asiwafuate nyumbani kwa binti yake, Kijitonyama, Dar ambako wanapika na kupakua, kilijibu:
“Ameweka mtego wake pale, bahati mbaya sana Diamond naye anaishi kwa machale. Kuna siku anakwenda kulala kuna siku haendi. Huenda na yeye (Diamond) ameweka watu wake ndani kwa Wema wa kumpelelezea kama mama Wema atakwenda au ana dalili za kwenda.”
Chanzo kikaendelea: “Siku hizi Diamond anaweza kwenda kwa Wema, akaacha gari lake na kutoka na la Wema na kurudi kwake usiku sana.”
Paparazi wa GPL akiwa nyumbani kwa Diamond.
AMANI LAWASAKA WAHUSIKA
Baada ya kuzinyaka nyeti hizo, Amani liliamua kuutafuta ukweli ambapo Jumanne iliyopita lilimsaka mama Wema kwa njia ya simu lakini iliita bila kupokelewa.
Amani lilitumia simu zake mbili kumpigia mwanamke huyo.
Baada ya dakika tano, mama huyo mwenye ‘machungu’ na mwanaume yeyote anayemchezea bintiye alituma ujumbe mfupi wa maneno (SMS) akisema: Nipo msibani tuma sms. Pia akatuma sms kwenye simu ya pili akisema: Nipo msibani, ulikuwa unasemaje?
Amani lilimtumia madai yote kuhusu yeye kuanza kuwatafuta Wema na Diamond, pia likamjulisha kwamba kama anawatafuta kweli, muda huo, wawili hao walikuwa wapo chumbani kwa Wema hawajaamka.
Hata hivyo, mama Wema hakujibu meseji yoyote kati ya hizo mbili hali iliyotafsiriwa na Amani kuwa, uchungu wa msiba ulimuondolea uwezo wa mawasiliano.
Paparazi wa GPL akiongea na mlinzi wa Wema nyumbani kwake.
NYUMBANI KWA DIAMOND
Mapaparazi wetu walitia timu nyumbani kwa Diamond, Sinza-Mori na kukutana na mtu mmoja aliyedai ni mjomba wa staa huyo ambaye alidai Diamond Platnumz alitoka asubuhi na mama yake, Sanura Kassim kwenda Tegeta, Dar.
NYUMBANI KWA WEMA
Baada ya kutoka nyumbani kwa Diamond huku wakiamini Mbongo Fleva huyo kaenda Tegeta kama alivyosema mjomba mtu, mapaparazi walikwenda nyumbani kwa Wema.
Baada ya kugonga geti kwa dakika moja, alitokea mlinzi na mambo yalikuwa kama ifuatavyo;
Paparazi: Mambo?
Wema.
Mlinzi: Poa, karibu.
Paparazi: Asante, nina shida na Wema, sijui nimemkuta?
Mlinzi: Wamelala, hawawezi kuamka muda huu.
Paparazi: Wamelala? Nani na nani?
Mlinzi: Madam (Wema) na Diamond.
Diamond.



Paparazi: Ina maana Diamond yumo ndani?
Mlinzi: Si nimekwambia wamelala?
Paparazi wetu alifanikiwa kupenyeza macho kwenye nafasi ya uzio na kuyaona magari ya wote wawili, la Diamond aina ya Toyota Land Cruiser V8 na la Wema, Toyota Lexus Harrier.

YULE MCHUNGAJI ANYEZITOLEA MACHO MALI ZA MAREHEMU KULOLA, AKUMBANA NA JOTO YA JIWE KUTOKA KWA WATOTO WA MAREHEMU.

SHETANI ana majaribu yake! Anaendelea kuifuatilia familia ya mtumishi wa Mungu aliyekuwa Askofu Mkuu wa Kanisa la Evangelist Assemblies of God Tanzania (EAGT), Marehemu Dkt. Moses Kulola.
Habari za karibuni, mpasuko mkubwa umeibuka baada ya kuwepo kwa sintofahamu dhidi ya mirathi ya marehemu huyo aliyefariki dunia Agosti 29, mwaka jana huku makundi mawili yakiibuka.
Awali, Mchungaji Katunzi aliibuka na kudai kuwa yeye ndiye msimamizi wa mirathi ya ambapo tamko hilo lilipingwa na baadhi ya wanafamilia.
Kwa mujibu wa chanzo makini, hivi karibuni Katunzi alitimuliwa nyumbani kwa marehemu Kulola akiwa amepeleka mchele na pesa taslimu shilingi laki tatu (300,000) alizodai ni sadaka kwa mjane wa marehemu.
Mchungaji wa Kanisa la EAGT City Center, Florian Katunzi.
“Hivi karibuni Mchungaji Katunzi alikwenda kwa mjane wa marehemu akatimuliwa, walidai ni msaliti mkubwa wa familia.
“Wakati akitimuliwa nyumbani hapo maeneo ya Capripoint, Abel (mtoto wa marehemu) naye alimshambulia mchungaji huyo na kumwambia asirudi tena nyumbani kwa marehemu kwani amekiuka miiko ya uchungaji ya kiapo cha uaminifu,” kilisema chanzo chetu na kuomba hifadhi ya jina.
Pia kiliongeza: “Familia kwa sasa ina mpasuko mkubwa, kuna makundi mawili, wapo wanaomuunga mkono Mchungaji Katunzi na wasiomuunga.
“Kundi linalomuunga mkono linaongozwa na watoto wawili wa marehemu (majina tunayo).
Kundi jingine ni la mjane wa Kulola, Elizabeth Kulola linaundwa na watoto wa marehemu wakiongozwa na Abel aliyekuwa dereva wa marehemu, Mchungaji Dany, Goodluck, Mary, Anna, Janga Faith na Susan.
Mke wa marehemu Moses Kulola.
Mchungaji Dany Kulola kwa sasa yuko Marekani na inasemekana kuwa amechukizwa sana na kitendo cha ndugu wanaomuunga mkono Katunzi.
Marehemu Kulola alikuwa na watoto 13, waliofariki dunia ni Flora, Benjamin na Rachel.
Wosia wa marehemu uliopatikana hivi karibuni unaonesha kuwa, mjane wa marehemu ndiye mrithi halali wa mali zote.
Habari zaidi zinasema Katunzi ameshaitwa na wachungaji wa Kanisa la EAGT ngazi za juu na kumtaka ajitoe katika sakata hilo la mirathi lakini anaendelea kufuatilia.
Habari nyingine kuhusu sakata hilo zinasema kuwa, Jumapili iliyopita akina mama 150 wa Kanisa la EAGT Jimbo la Mwanza walikwenda nyumbani kwa marehemu baada ya kusoma habari kwenye Gazeti la Risasi Jumamosi Toleo Namba 1074 la Januari 25-28, 2014 likiwa na kichwa cha habari; Mgogoro Mzito Mirathi ya Kulola.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, akina mama hao walimuombea mjane wa marehemu huku wakimshutumu vikali Katunzi kwa kufanya jaribio la kumpeleka mahakamani mama Kulola kabla ya kufanyika kwa kikao cha ukoo na kuona nani anaweza kuwa msimamizi wa mirathi hiyo.
Mjane wa marehemu alipozungumza na gazeti hili alikuwa na haya ya kusema:
“Familia yangu ina mpasuko mkubwa, watoto wangu hawaelewani na Katunzi, nimepata mfadhaiko kuhusu mambo ya familia kuanza kuhusishwa na mahakama, watoto wangu siku hiyo walipomfukuza Katunzi nyumbani niliwagombeza sana kwani halikuwa jambo la kawaida.
“Kwa sasa mambo yote namwachia Mwenyezi Mungu, wote ni watoto wangu siwezi kuwabagua hata siku moja. Kinachosumbua hapa ni kila mmoja kuwa na tamaa ya mali za kidunia. Haya yote ni majaribu ya mwovu shetani.”



Jumatatu iliyopita, saa 2:56- 58 asubuhi, Mchungaji Katunzi hakupokea simu ya mwandishiili kujibu madai ya kuwa aliwahi kutimuliwa na baadhi ya watoto wa mzee Kulola kama chanzo chetu cha habari kilivyodadavua.
Blogger Widgets