Showing posts with label Udaku wa Tanzania. Show all posts
Showing posts with label Udaku wa Tanzania. Show all posts

Monday, February 3, 2014

LADY JAY DEE ADAI TALAKA KWA GARDNER, SOMA KISA KIZIMA HAPA.


UNAWEZA ukakataa lakini ndivyo ilivyotokea, ndoa ya mtangazaji mahiri Bongo, Gardner Gabriel Fikirini Habash ‘Kapteini’ na Mbongo Fleva, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ iliyofungwa miaka 9 iliyopita inadaiwa kuingia kidudu kufuatia mke huyo kuomba aandikiwe talaka, ni Ijumaa Wikienda pekee lenye uthubutu wa kuripoti mkasa wote.
Jide akiwa na jumewe Gardner.
Kwa mujibu wa chanzo chetu cha kuaminika, Jide au Lady Jaydee alifikia uamuzi huo baada ya Gardner kupata kazi ya kutangazia redio moja nchini Kenya.
HABARI KAMILI
Mnyetishaji wa kisanga hiki, aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa mara baada ya mume huyo kupata mchongo mzima alirudi nyumbani akiwa na furaha na kumwambia mkewe kuhusu bahati hiyo.
“Baada ya Gardner kupata mchongo wote wa kazi alikwenda mbio nyumbani kwake Kimara (Dar) ili akamwambie mkewe.
“Pia katika safari ya kwenda Kenya kupiga mzigo ilikuwa aende na mkewe huyo kwa sababu lilikuwa suala la kuhamisha makazi yao Tanzania,” kilisema chanzo hicho.
Jide na Gardner siku ya ndoa yao.
JIDE AHAMAKI
Chanzo kikatoboa kwamba Gardner alipofika nyumbani kwake na kumweleza mkewe, alikumbana na kitu ambacho hakukitarajia.
“Komando (Jide) alihamaki na kumjia juu akisema yeye hawezi kuondoka Tanzania kwenda kuishi Kenya, kama Gardner analiona jambo hilo ni heri kwake, amuandikie talaka yake na kuachana ili kila mmoja achukue hamsini zake,” chanzo kilizidi kuporomosha maneno.
KWA NINI JIDE HAKUPENDA? 
Habari zilizidi kuanikwa kwamba Jide au Binti Machozi alifikia uamuzi huo baada ya kugundua kuwa kitendo cha kwenda kuishi Kenya kitaua bendi yake ya Machozi na sehemu ya biashara ya Nyumbani Lounge iliyopo Ada-Estate, Kinondoni, Dar.
MBAYA ZAIDI
Taarifa zikazidi kumiminika kwamba, mbali na Jide au Anakonda kuhofia biashara zake kufa, lakini pia hakupenda Gardner aondoke hata peke yake kwa sababu yeye ndiye meneja wa miradi hiyo miwili.
“Mimi nilipopata habari hizo nilikutana na Jide nikamuuliza, akanijibu ameamua iwe hivyo tu, kikubwa mumewe (Gardner) aamue moja kati ya hayo mawili kwani yeye ana haki akiwa kama mkewe wa ndoa,” kilisema chanzo kikimkariri Jide.
GARDNER AISHIWA NGUVU
Kufuatia majibu ya mkewe, taarifa zinasema mtangazaji huyo ambaye alishawahi kupiga mzigo kwenye kituo cha Radio Clouds FM cha jijini Dar alijikuta akiishiwa nguvu na kuachana na dili hilo mara moja.
“Gardner alisalimu amri kwa mkewe, akaamua kuachana na dili la kwenda kutangaza Kenya. Lakini alifikiri sana akasema ni kweli kuhamia Kenya kungeua miradi yao ya Tanzania maana ingekosa msimamizi wa kuaminika,” chanzo kiliweka wazi.
KAMA ANGEKWENDA KENYA
Siri hiyo iliyovujia mikononi mwa Ijumaa Wikienda haikuishia hapo, ilizidi kuanikwa kwamba kama Kapteini angekwenda Kenya na kuanza kazi, ilikuwa alipwe mshahara wa shilingi za Kenya laki 3 kwa mwezi (kama milioni 6 za Tanzania).

NAFASI YAKE BADO IPO
Mpashaji wetu alisema kwamba nafasi ya Gardner kwenye kituo hicho cha redio ambacho hakikutajwa, bado ipo lakini tamko la Jide nalo li hai, kwa vile hakubatilisha, endapo mumewe atataka kwenda hata kesho (Jumanne) aandike talaka.
WIKIENDA NA GARDNER
Baada ya kunyetishiwa taarifa nzima, juzi gazeti hili lilimsaka Gardner. Kwa njia ya simu lilimkosa, likamfuata Nyumbani Lounge. Lilipomkuta lilimsimulia kisanga chote cha ndoa yake kutikiswa na kitendo cha yeye kupata kazi Kenya ambapo alijibu hivi:
“Ndoa ni nzuri, ni kweli ilikuwa niende Kenya, nilipata kazi kule lakini kama familia ilikuwa lazima tukae na kupanga, mwenzangu hakuafiki.”
Wikienda: “Ni kweli shemeji ameomba uchague mawili, umwandikike talaka au uende Kenya?”
Gardner: “Ndiyo maana nimesema ndoa nzuri, lazima makubaliano yawepo, mke anaweza kuonesha msimamo wake na mume kama utakaa chini na kuufikiria ukapata jibu unakubaliana na mke wako wala hakuna ubaya.”
Wikienda: “Kule mshahara wako ungekuwa shilingi ngapi?”
Gardner: “Hiyo sasa ni siri ya makubaliano.”
Wikienda: “Kwa nini usiamue kwenda tu?”
Gardner: “Nimekwambia ndoa nzuri.”
JIDE BIZE
Juhudi za kumpata Jide ziligonga mwamba baada ya muda wote kuwa bize na shoo ya kukata na shoka aliyokuwa akiifanya siku hiyo kwenye ukumbi huo akikimbiza na nyimbo zake kali za zamani na hizi mbili zilizogeuka nyimbo za taifa, Joto Hasira na Yahaya.
RAFIKI WA GADNER AMCHAMBUA JIDE
Rafiki wa karibu na Gardner (jina tunalo) ambaye alisikia mahojiano ya mtangazaji huyo na Ijumaa Wikienda, alisubiri jamaa aondoke ambapo alianza kumchambua Jide.
“Nataka kuwaambia kitu, Jide ni mwanamke jasiri sana. Ana msimamo na anaposhikilia msimamo wake hatengui hasa kama atabaini kuwa yupo sahihi.
“Ni kweli jamaa (Gardner) alipata kazi Kenya tena mshahara mzuri tu, lakini mama (Jide) akaweka ngumu hakuna kwenda,” alisema rafiki huyo.
GPL

LOL!! KUMBE YULE MCHUMBA WA KIZUNGU WA SHILOLE " NI SHOGA" AKA MCHICHA MWIBA.


Yeleuuuwi! Siku chache baada ya msanii wa sinema na muziki Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ kujinadi na mchumba wa Kizungu aliyejulikana kwa jina moja la Ankar, siri imefichuka kwamba jamaa huyo ni mwanaume tata.
POZI TATA: Ankar katika pozi.
Kikizungumza na Ijumaa Wikienda kutoka London, Uingereza, wikiendi iliyopita, chanzo hicho makini kilisema mwanaume ambaye hivi karibuni Shilole alijinadi kuwa ni bwana’ke siyo kwani huko London baadhi ya watu wanamfahamu kama mwanaume tata kijinsia.
MAUNO: Ankar akikata mauno.
“Yule jamaa anapenda sana kukaa na wanawake, sijawahi kumuona na wanaume wenzake, kazi kukata tu mauno na wanawake. Nilishangaa sana Shilole kusema eti ni mchumba’ke wakati hapa London (Uingereza) ni maarufu sana kwa kushiriki pati za wanawake.
WAPENZI: Zuwena Mohamed ‘Shilole’ akiwa na 'mchumba wake', Ankar.
“Maskini Shilole, pale imekula kwake, hakuna chochote,” kilisema chanzo hicho.
Baada ya kunyetishiwa habari hizo, gazeti hili lilimtafuta Shilole ambapo alikuwa na haya ya kusema:
PIPI YA KIJITI: Ankar akifyonza pipi ya kijiti.
“Jamani imeniuma sana kwani nilikuwa sijui, nimeligundua hilo baada ya kuambiwa na watu, nilipigiwa simu kutoka Uingereza kwamba yule mwanaume siyo hivyo sina mpango naye tena kwa kweli,” alisema Shilole anayetamba na kideo cha Nakomaa na Jiji.
TABASAMU: Ankar akitabasamu katika pozi.

GPL.

WEMA NAE KAVURUGWA, ETI AKIFA AAGWE UWANJA WA TAIFA MAANA LEADERS HAPATA TOSHA.


Kazi ipo! Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu ambaye huwa haishiwi habari, ameibuka na jipya akidai kuwa akifa leo au kesho basi aagwe Uwanja wa Taifa jijini Dar, Ijumaa Wikienda limemtegea sikio.
Wema Isaac Sepetu.
Miss Tanzania huyo wa 2006/07 ambaye anakimbiza kwenye sinema za Kibongo alifunguka hayo wikiendi iliyopita wakati akiwa safarini kuelekea jijini Arusha ambapo msanii anayemilikiwa na kampuni ya Wema ya Endless Fame Production aliyetajwa kwa jina moja la Mirrow alikwenda kuangusha shoo pande hizo.
Wema aliyasema hayo alipokuwa akichangia mada ya utabiri wa mtoto wa aliyekuwa mtabiri bingwa, marehemu Sheikh Yahya Hussein, Maalim Hassan Hussein aliyetabiri kwamba wasanii wengi wenye majina makubwa watakufa mwaka 2014.
Mwanadada huyo alisema mastaa wengi wameaga dunia na kuagwa kwenye Viwanja vya Leaders, Kinondoni lakini yeye itakuwa Uwanja wa Taifa.
Alitolea mifano ya waliokuwa mastaa kama Steven Kanumba, Albert Mangweha ‘Ngwea’, Julius Nyaisangah ‘Anko J’ na wengine kuwa waliagwa Leaders lakini kwa namna ambavyo jina lake ni kubwa ndani na nje ya Bongo viwanja hivyo havitatosha.
“Mimi nakwambia kabisa, pale Leaders hapatatosha. Kama nikifa leo au kesho, niagwe Uwanja wa Taifa ili kila mtu apate nafasi. Naamini watu watakuwa wengi sana so Leaders hapatatosha,” alisema staa huyo mkubwa anayeminya kilamalavidavi na Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
Ijumaa Wikienda lilipododosa kwa marafiki zake wa karibu lilitonywa kwamba tayari jambo hilo alishawaeleza na kwamba aliomba iwe hivyo.
Mbali na wasanii, Maalim Hassan alitabiri pia kuwa mwaka huu kuna mwanasiasa mkubwa atakufa na utakuwa msiba wa kitaifa, vifo vya wanahabari na malumbano makubwa juu ya serikali tatu.
Wiki iliyopita ilijaa simanzi baada ya kufariki dunia kwa watu maarufu kama mchekeshaji wa Futuhi ya Star TV, Omary Majuto ‘Mzee Dude’, mpiga ngoma wa Bendi ya The African Stars ‘Twanga Pepeta’, Soud Mohamed ‘MCD’, mwigizaji wa Bongo Movies, Victor Peter na mtangazaji wa East Africa Radio, Kenneth Kidago Lyanga.

GPL.

CCM YAWATEKA WASANII WA BONGO MOVIES, MAMIA WAJIUNGA RASMI.


Chama cha Mapinduzi (CCM) kimefanikiwa kupata wanachama wapya ambao ni wasanii wa tasnia mbalimbali, miongoni mwao ni Uwoya, Johari, Banana, JB na Mrisho Mpoto.

Chanzo: Jamii FORUMS

SNURA ALIA NA WABAYA WAKE, WANAOTAMANI AANGUKE.


STAA aliyeliteka soko la mduara kwa kibao chake cha Majanga, Snura Mushi amesema watu wenye chuki na yeye wamepanga njama za kumshusha kwenye chati kutokana na maendeleo yake.
Snura Mushi.
Akipiga stori na paparazi wetu juzi, Snura alisema: “Nashangaa sana ninapofanya jambo zuri halafu watu wanaligeuza kuwa baya ili nichafuke jina na kunipunguzia mvuto kwa mashabiki wangu.”
Chanzo cha yote ni baada ya mwanadada huyo kupiga shoo kwenye Ukumbi wa Buliyaga, Temeke, Dar siku chache zilizopita, kundi la watu wasiojulikana walianza kueneza taarifa kuwa alifanya vibaya na mashabiki wakamtaka ashuke jukwaani jambo ambalo alisema halikuwa na ukweli wowote.

RAYUU BADO ANATAMANI KUTEMBEA NA MUME WA MTU, ASEMA HAWEZI KUJIZUIA.


MSANII kinda kwenye tasnia ya filamu Bongo, Rahma Bagenzi ‘Rayuu’ amesema kuwa, kamwe hatokoma kutembea na waume za watu kwa kuwa sheria ya dini yake ya Kiislamu inamruhusu kuolewa na mume wa mtu.
Rahma Bagenzi ‘Rayuu’.
Akipiga stori na paparazi wetu, Rayuu alisema kipindi cha nyuma aliwahi kutoka kimapenzi na mume wa mtu (hakumtaja jina) na kufikia hatua ya kufikishwa polisi na mwenye mke lakini haimaanishi kuwa hatatembea tena na mume wa mtu.
“Nikila kiapo cha kutotembea na waume za watu nitakuwa naongopa, kwanza dini yetu imeruhusu ndoa za uke wenza huenda  Mungu kaniandikia niolewe ndoa ya aina hiyo sina uwezo wa kupingana naye,” alisema Rayuu.

GPL.

DR CHENI APANIA KUIRUDISHA KAOLE SANAA GROUP.


MWENYEKITI Msaidizi wa Bongo Movie Unity, Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’ amesema amekumbuka na kutamani kurudisha Kundi la Sanaa ya Maigizo la Kaole ‘Kaole Sanaa Group’ liwe na nguvu kama zamani.
Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’.
Dk. Cheni alisema japo kundi hilo limeonekana kupoteza mvuto wake wa awali, lakini anaamini wasanii wengi wanaofanya vizuri kwenye tasnia ya filamu kwa sasa wametoka katika kundi hilo maarufu.
Hata hivyo, pamoja na kupotea kwa kundi hilo, Dk. Cheni anatamani sana kulirejesha kwenye ulingo wa sanaa na kwamba kuna mikakati anayoiandaa ili kukamilisha azimia hiyo.
“Naitamani Kaole ya zamani, nahisi kama kuna vionjo vinakosekana siku hizi. Wasanii wengi wenye majina makubwa kwa sasa wametoka kwenye kundi hilo, lakini nitajitahidi kulirudisha, naamini nitafanikiwa,” alisema Dk. Cheni.

BAADA YA KUJIINGIZA KIAINA NA SIASA, WANA BONGO MOVIES WAMTAKA STEVE NYERERE AJIUZULU.


Hali si shwari katika klabu ya wasanii wa filamu za Kibongo, Bongo Movie Unity ikidaiwa kuwa baadhi ya ‘memba’ wake wanashinikiza mwenyekiti wake, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ ajiuzulu.
Steven Mengere ‘Steve Nyerere’.
Habari zilizoifikia Stori Extra wikiendi iliyopita zilidai kuwa, baadhi ya wasanii wa klabu hiyo akiwemo mwenyekiti huyo walilamba mshiko kutoka kwa mwanasiasa mmoja wa CCM mkoani Mbeya ili wamfanyie kampeni katika uchaguzi ujao jambo ambalo wenzao walilipinga vikali kwa kuwa wao hawajihusishi na siasa bali wasanii na jamii.
Alipotafutwa Steve kujibu tuhuma hizo hakupatikana lakini katibu wake, William Mtitu alikiri kuwepo kwa ishu hiyo.
GPL.

Friday, January 31, 2014

GURUMO AFAGILIA DIAMOND PLATINUMZ KWA KUWAKAMUA WATOTO WA KIKE TOFAUTI TOFAUTI, ADAI WANAJIPELEKA WENYEWE.


MSANII mkongwe wa muziki wa dansi Bongo, Muhidini Gurumo ambaye kwa sasa amestaafu, amefungukia skendo ya kuwa na mademu wengi inayomuandama Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Akipiga stori na Ijumaa hivi karibuni maeneo ya Ilala jijini Dar, Mzee Gurumo alisema: “Diamond ana nidhamu sana ila vile anavyotamba jukwaani na kudatisha mashabiki hapo ndipo balaa linapokuja, watoto wa kike wenyewe wanaanza kujisogeza kwake.
Mzee Muhidini Gurumo.
“Pamoja na skendo za mademu zinazomuandama, siwezi kumshusha thamani, ana haki ya kujiopolea mwanamke yeyote anayempenda, yeye kama mwanaume rijali wakati mwingine ni vigumu kujizuia na vishawishi hivyo.”
GPL.

KILA MTU NA "ULEVI" WAKE, JE WAJUA STAREHE YA WASTARA NI NINI?!!!!


MSANII wa filamu, Wastara Juma amefunguka kuwa starehe yake kubwa duniani ni kukumbatiwa na anapofanyiwa kitendo hicho na mtu wa jinsia yoyote huwa hoi.
Wastara Juma.
Akistorisha na paparazi wetu, Wastara alisema: “Mimi napenda sana kukumbatiwa au kukumbatia, awe ni mwanaume au mwanamke, ndugu yangu au hata kama siyo ndugu yangu, tukikumbatiana tu najisikia raha sana.
“Unajua kila mtu anakuwa na kitu anachokipenda duniani sasa mimi starehe yangu ndiyo hiyo hata marafiki zangu wanajua kwamba mimi napenda kukumbatiwa.”

BASATA "WAMVURUGA" SNURA MAJANGA


KATIKA toleo namba 859 la Desemba 29 hadi Januari 2, 2014 la gazeti hili, kwenye safu yetu hiihii, niliandika kuhusu Snura Mushi, msanii anayetingisha anga la muziki wa mduara. Yupo juu kwa kuwa kibao chake cha Majanga kinasumbua mno hivi sasa.
Snura Mushi.
Kwa wale ambao hawakubahatika kunisoma, niliandika nikionyesha masikitiko yangu kwa namna binti huyu anavyocheza akiwa jukwaani na hata kwenye video zake.
Kama haujawahi kumuona akiwa jukwaani, ni kwamba Snura anajua hasa kukichezea kiuno chake, ni mjuzi wa kukizungusha kwa namna ya kuburudisha kabisa na hatari zaidi, pale anapoamua kuwapa mgongo mashabiki walio ukumbini, kisha akawatingishia kwa namna ya kutetemesha makalio yake makubwa!
Ni aina ya uchezaji ambao kwa watu wazima, ni burudani mno, hasa kama wakati huo, tayari wale wa kiburudisho wanakuwa wamepata moja mbili. Uchezaji wake unaleta mfadhaiko zaidi hasa kutokana pia na uvaaji wake. Amechagua kuwa mtu mwenye mavazi tatanishi.
Lakini kama baba au mama waliostaarabika, hawawezi kujisikia vizuri kumuona msichana huyu akiwajibika jukwaani wakiwa na watoto wao, bila kujali kama ni wasichana au wavulana. Ni aibu, kinyume cha maadili na tena, hamna chochote ambacho watoto wadogo wanaweza kujifunza.
Katika habari ile, niliwashauri pia Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), baada ya kuwa wamefanikiwa kupunguza ujinga wa waigizaji wa filamu wavaa nusu utupu, kuanza kukagua pia video za wasanii wa muziki wa kizazi kipya, kwani wapo wengine wanaojaribu kujitoa ufahamu, wakivaa Kimarekani wakati tunajua wazi kwao ni Kilosa.
Ni jambo linalotia faraja kuja kusikia kuwa BASATA, limeipiga marufuku video ya Snura ya wimbo wake mwingine, Nimevurugwa. Sijawahi kuiona video hiyo, lakini kwa namna ninavyomfahamu msanii huyu anavyoshughulika akiwa jukwaani, ni rahisi kuelewa kilichomo unaposikia kuhusu kuzuiliwa kwake.
Nichukue nafasi hii kuipongeza sana Basata, lakini wakati huohuo kutoa wito kwa chombo hicho cha serikali, kuangalia kwa jicho kali zaidi nyimbo nyingine zinazopigwa katika vituo vyetu vya televisheni, kwani wameruhusu ‘uzungu’ usio na maana kwa jamii, kana kwamba watu wanafuata maungo ya wacheza shoo badala ya kusikiliza ujumbe.
Inasikitisha kuona kwamba licha ya uchezaji huo wa kujidhalilisha, bado kuna msanii mwingine naye amemuiga karibu kwa kila kitu. Naye amekuwa akicheza na kuvaa kwa namna inayowadhalilisha sana mama zetu, lakini kwa namna ya kushangaza, wenyewe wamekuwa wakijisikia fahari na kuamini wanavutia.
Nimekuwa nikisema mara kwa mara kwamba wasanii wetu, hasa wale wanaobahatika kuwa nyota kwa kazi zao, wanapaswa kuwa mfano mbele ya jamii. Wanatakiwa wajue kuwa miongoni mwa mashabiki wa kazi zao, ni watoto wadogo, dada, kaka, shangazi na wazazi wanaojiheshimu. Unajaribu kujiuliza, hivi Snura anaweza kukata mauno kwa jinsi ile mbele ya wazazi wake?
Kwa vyovyote jibu la swali hili litakuwa ni hapana, vinginevyo labda awe na matatizo yasiyo ya kawaida kwenye kichwa chake. Sasa kama hawezi kucheza namna ile mbele ya wazazi wake, anajisikiaje anapofanya vile mbele ya wazazi wa wenzake?
Ni kweli biashara ni ubunifu, lakini inapendeza zaidi ubunifu wetu ukazingatia pia maadili yetu kama jamii yenye kuheshimiana. Uchezaji wa Snura jukwaani, unatoa ushawishi mkubwa kwa shabiki anayemsogelea kumshika makalio.
Mimi bado ni shabiki mkubwa wa maadili na ninaamini kutoka moyoni kwamba mashabiki wa muziki wa kizazi kipya wanavutiwa zaidi ya tungo kuliko uvaaji wa nusu uchi jukwaani.
Snura, Shilole na wasanii wengine wanaovaa na kucheza kihasara hasara, wanapaswa kubadilika kwa faida ya watoto wetu ambao utandawazi unaonekana kuwapoteza zaidi badala ya kuwasaidia!
GPL.

Wednesday, January 29, 2014

HATIMAYE SHILOLE ANASA KWA MCHUMBA WA KIZUNGU.

KWA mara ya kwanza msanii wa filamu na muziki Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amenaswa akiwa na mwanaume wa Kizungu anayedaiwa kuwa ndiye mchumba wake.
Zuwena Mohamed ‘Shilole’ akiwa na mchumba wake.
Chanzo makini kimepenyeza habari kuwa, safari za mara kwa mara za Shilole nchini Uingereza zimekuwa zikisababishwa na mchumba huyo wa Kizungu ambaye huwa anamuita kufurahia p#nzi lao pamoja na kumtafutia shoo mbalimbali.
“Ukweli ni kwamba Shilole ana mchumba wa Kizungu na walikutana kwenye shoo ya mara ya kwanza aliyoenda kufanya nchini Uingereza na hivi karibuni ataenda tena na amealikwa na huyo mchumba wake,” kilisema chanzo hicho.
Gazeti hili limekuwa la kwanza kunasa picha kadhaa za Shilole akiwa katika mapozi tofauti ya kimahaba na Mzungu huyo.
Baada ya chanzo hicho kumwaga ‘upupu’ huo, mapaparazi wetu walimtafuta Shilole ili aweze kufunguka ambapo bila kuumauma maneno, alikiri kuwa amepata mchumba huyo aliyemtambulisha kwa jina la Ankar.
Akizidi kumwaga data za boifrendi wake huyo, Shilole alisema awali walikutana kwenye moja ya shoo zake nchini humo ndipo urafiki ulipoota mizizi na kufikia hatua ya kuwa wap#nzi.
“Kweli nina mchumba Mzungu ambaye ni raia wa Uingereza, nilipokuwa napataka nimefika, sipindui tena. Unajua muziki wangu na mauno yangu yanawavutia sana watu, siku ya kwanza aliniona kwenye shoo akanipenda ndipo tukaanzisha urafiki.



“Hivi karibuni nina safari ya kwenda nchini humo kwa mwaliko maalum alionipa, nitaenda peke yangu kwani safari nyingine zote zilizopita nilikuwa naenda na watu,” alisema Shilole.

WATOTO 6 KWA MAMA TOFAUTI WAMFILISI DUDE, AKOSA PESA YA KUREKODI TAMTHILIYA YAKE.

HALI ya uchumi ya mwigizaji Kulwa Kikumba ‘Dude’ imemkwamisha mwigizaji huyo ashindwe kurekodi tamthiliya yake.
Kulwa Kikumba ‘Dude’.
Akizungumza na paparazi wetu, Dude alikiri kuwa uchumi umemkalia vibaya ambapo aliruhusiwa kupewa muda wa hewani katika Runinga ya East Africa lakini akashindwa kushuti kutokana na majukumu ya kifamilia kumuandama.



“Daa we acha tu, mwezi wa kwanza huu majanga matupu. Nimeshindwa, kama unavyojua nina watoto wengi mambo ya ada yamenibana kwelikweli,” alisema Dude ambaye ana jumla ya watoto sita kwa mama tofauti.

MIMBA ILIVYOMNYIMA "DILI" ZA HELA DAVINA WA BONGO MOVIES

STAA wa Bongo Movie, Halima Yahaya ‘Davina’ amefunguka kuwa mwaka 2013 aliutumia zaidi kwa kulea mimba hadi kujifungua hivyo kukosa madili ya kazi za uigizaji.
Halima Yahaya ‘Davina’.
Akizungumza na paparazi wetu, Davina alisema mwaka huu amejipanga kurejea upya katika sanaa kwani amegundua kuwa mashabiki wake walikuwa wamemmisi hivyo lazima apambane kutetea taito yake katika sanaa.



“Nimejipanga zaidi mwaka huu, nimedhamiria kufanya mapinduzi makubwa katika sanaa tofauti na kipindi cha nyuma, kulea siyo mchezo ilibidi sanaa ikae pembeni kidogo,” alisema Davina ambaye sasa ni mama wa mtoto mmoja, Fazal.

Tuesday, January 28, 2014

MASTAA WA BONGO MOVIE WAMPONDA WEMA SEPETU BAADA YA KUNYANG'ANYWA KILA KITU NA MP#NZI WAKE KIGOGO WA SERIKALINI.


MASTAA wa kike Bongo wamecharuka na kutoa yao ya moyoni baada ya nyota mwenzao, Wema Sepetu kubwagwa na aliyekuwa mpenzi wake, anayetambulika kwa jina moja la Clement na kumnyang’anya vitu alivyompa kama zawadi wakati wa mapenzi yao.
Wema Sepetu.
Kuhusu Wema kuporwa ofisi yake ya Endless Fame Film Production, kupewa notisi ya nyumba aliyokuwa amepangiwa na kigogo huyo anayeelezwa yupo serikalini na kunyang’anywa magari siyo stori kabisa mjini.
Risasi Mchanganyiko lilifanya mahojiano na mastaa hao wikiendi iliyopita, kwa njia ya simu na kuwahoji kuhusu kitendo alichofanyiwa mwenzao ambapo walifunguka bila wasiwasi wowote.
USENGENYAJI
Wakali hao, waliopata kuzungumza na waandishi wetu kwa nyakati tofauti, baadhi wamemponda Wema kwa kutokuwa makini wakati akiwa kwenye uhusiano na kigogo huyo kwa kutaka kukabidhiwa hati za vitu alivyopewa.
Wa kwanza kuzungumza ni Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ ambaye alisema: “Mimi namshukuru Mungu kwa sababu sijapangiwa nyumba na mwanaume.  Naishi maisha yangu simpo ya furaha na amani, sipendi kuigiza maisha. Hao wasanii wanaopenda mambo makubwa wakati hawana uwezo,  nawashauri wafanye kazi, filamu zinalipa sana. Wasipende vitu vya haraka, maana siku zote vizuri huja taratibu.”
ZUWENA MOHAMED ‘SHILOLE’
“Mastaa tusijiachie sana kwa wanaume, kama ukipewa gari, upewe na kadi... tusidanganyike na tusipende kuhongwa, tutafute vya kwetu. Kama mtu anakupenda na anakusaidia kwa mapenzi mema, sawa mheshimu.”
WASTARA JUMA
“Inabidi tujitambue jamani, maana kuna watu wanatembea na mastaa makusudi ili wajulikane au kwa manufaa yao wenyewe. Tuache kuishi kwa kutegemea migongo ya wengine. Wengi hawana mapenzi ya kweli. Hata kama mmeachana, sasa kuna sababu gani ya kumnyang’anya mtu vitu ulivyompa?”
NURU NASSOR ‘NORA’
“Mimi najisikia vibaya sana... kama mtu unajiamini una kipaji, kwa nini usifanye kazi?  Mastaa tuache kujitangaza, kwa sababu tunatumika kama vyombo vya starehe tu.  Tutafute ndoa, tusitumie ustaa kufanya ufuska kwa sababu mali zinapita na mwisho wa siku tunaharibu maisha yetu.”
TAMRINA POSH ‘AMANDA’
“Utapeli ni mwingi, haya mambo ya kupewa vitu siyo vizuri kabisa, tuache.  Wanawake tuna akili fupi sana na tunajisahau tunapokuwa na wanaume wakati wenyewe wana kitu moyoni mwao, akishapata anachotaka anaanza matatizo.



“Bora nitembelee taksi au Bajaj kuliko kudhalilishwa... wanawake ni wajinga na huwa tunajidanganya kwa vitu visivyo vyetu, mwisho wa siku tunaumbuka. Tuache sifa za kijinga.”
Blogger Widgets