Saturday, March 30, 2013

"Mauno" ya Aunt Lulu Yamzimisha Njemba Shughulini

-->
Mwanadada Lulu Mathias Semagongo Juzi juzi alimfanya jamaa mmoja kuzimia katika harusi ya bibie jack baada ya mwanadada huyo kukata kiono mpaka jamaa akapatwa na kizunguzungu na hatimaye kudondoka chini na kuzimia. Kioja hicho kilichovuta hisia za wengi kilitoka baada ya mwanadada huyo aliyebeba mzigo wa maana alipoamua kufanya kweli katika sherehe hiyo na ndipo miongoni mwa njemba zillizokuwepo hapo kuamua kuunga tela...... huku akiwa na sahani yake ya chakula mkononi mara "puuuh" chiniiii.-->

Udaku Wa Magazetini

-->

Thursday, March 28, 2013

Sinta, Dida na Mange ndani ya Bifu zito.

--> Kama mdau wa mambo ya udaku nakuomba tembelea blog ya www.irenemwamfupejamii.blogspot.com na www.Sintah.com utajionea mwenyewe jinsi gani warembo hawa wanavyotafutana na siku si nyingi watatoana macho hapa mjini. miongoni mwa articles zilizomo ni hii ya Mange" I THINK WENGI WETU TULIAMUA KUMU IGNORE TU HUYU MBWA KOKO......KAMA MIMI NDO KABISAAAAA YANI NILIKUWA NISHASEMA NGOJA NIFANYE KAMA HAYUPO HAI...... JAMANI
KILA SIKU LAZIMA ANITUKANE KWENYE COMMENTS ZAKE? NILIM CONTACT KISTAARABU NIKAMWAMBIA SINTA ACHANA NA MIMI, SIKUJUI TUHESHIMIANE, ILA WAPI JITU HALIELEWI.
SIJUI BLOG YAKE HAINOGI BILA KUMTAJA MANGE KIMAMBI. ALAFU UKILIAMBIA ETI LINASEMA SIO MIMI NAWEKA COMMENTS NI ADMINISTRATOR. SURA KAMA ADMINISTRATOR UNA HELA YA KUWEKA ADMINISTRATOR WEWE. MFYUUUUU.....

MIJITU MINGINE BWANA, YANI LAST WEEK NILIBOREKA KIDOGO NKAMZABUE VIBAO. JITU LINAJUA KABISA STORY NI ZA UONGO SASA ANAWEKA COMMENTS ILI IWAJE? BORA HATA BASI ANIFATE FATE MIMI, SOMETIMES ANAWEKA HATA COMMENTS ZA KUTUKANA
WATU AMBAO HATA HAWAJUI JUST BECAUSE HAO WATU WANA ISSUE NA MIE. YANI LAST WEEK NILISEMA NGOJA NKAMZABUE MABAO TUTAHESHIMIANA NIKAPELEKWA HADI KWAKE KANAKAA SINZA PALE BAMAGA, YANI HAPO ANAPOKAA TU NILIMUONEA HURUMA. NKAONYESHA NA HICHO KIBIRITI CHAKE ANACHOENDESHA, YANI NIKASEMA MASKINI YA MUNGU ADHABU TAYARI ANAYO SINA HAJA HATA YA KUMUONGELESHA....KHA!!!
WATU MNAAMBIWA MASHAUZI YANATAKA PESA HAMSIKIIII, MTU UNAJISHAUA WAKATI HUNA MBELE WALA NYUMA, UUNACHEKESHA WALIONUNA TU.UNAJISHAUA NA VINGUO VYA MTUMBA??? MFYUUUUUU, SHENZI KABISA....YANI NAONA HATA AIBU NIMEKAA HAPA NAANDIKA ARTICLE YA YULE MJINGA. ILA LAKINI MTU HAONI KWAMA ANAKUWA IGNORED, KILA SIKU ANANITUKANA ON HER BLOG BUT I IGNORE HER, HATA SIKU MOJA HUWEZI KUKUTA COMMENTS ZA YULE SINTA. HAJIULIZI KWANINI? ANAJIFANYA ANAJUA KUONGELEA MAMBO YA WATU YAKE TUKIONGELEA HAPA TUTAYAMALIZA?
SINTA KUBALI MAISHA YAKO, WEWE NI MTANZANIA WA KIMA CHA CHINI THATS UR STATUS NA SIO MBAYA ,JUST JIKUBALI UNACHEKESHA SANA UNAPOANZA KUTAKA KUWA MATAWI WAKATI YOU DONT HAVE ANYTHING.
HUYU NYAU ALIKUTANA NA MDOGO WA RAFIKI YANGU KWENYE NDEGE ON HER WAY TO UGANDA. KATIKA MAONGEZI HUYO MTOTO AKAMWMABIA AMEFIKIA SERENA HOTEL NA BABAKE. BASI SINTA ASIENDE HADI SERENA HOTEL KUMFATA HUYO MDOGO WA RAFIKI YANGU, ETI NAOMBA KWENDA CHUMBANI KWAKO NIKAPIGE PICHA NIWEKE KWENYE BLOG. HIVI HUYU MTU ANA AKILI KWELI??? JAMANI KAMA HUKUBARIKIWA KUWA NA MAISHA YA JUU EMBU YAKUBALI YAKO TU.
WEWE SINTA KUTAKA KUSHINDA NA MANGE KIMAMBI NI SAWA NA KONDOO ATAKE KUSHINDANA NA SIMBA...CHIEF UTAKUWA UNATANIA....
YOU WILL NEVER BE ME, HATA KARIBU YANGU HUTOFIKA UTAKACHOWEZA KUFANYA NI KUNITUKANA KWENYE COMMENTS ALAFU UJIDAI ETI NI WATU WANANITUKANA....
MBWA MKUBWA MTU SINA BEEF NA WEWE, SIJAWHAI KUGOMBANA NA WEWE, UNANIFATAFATA NINI ?????? NISHAKWAMBIA KISTAARABU MARA MIA KIDOGO HUSIKIIII... ILA UNACHOKITAFUTA KWANGU UTAKIPATA... TENA SHUKURU SIKAI DAR ,
MAANA NIKIJA DAR NIPO BUSY KUTAFUTE MAHELA STAKI KUPOTEZA MUDA POLISI LA SIVYO NGEKUWA NISHAKUTENGUA KIUNO NYAU WE.

HIVI NA NYIE KINA DIDA NA WENGINE MNAOSUMBULIWA NA HUYU PANYA HIVI MNASHINDWA KUMFUNZA ADABU MTU MNAISHI NAE HAPA HAPA TOWN. SIKU MOJA MKAMATENI MUMPE KIBANOO MUMTOE NA NGUO MUMPIGE PICHA MNITUMIE NIWEKE HUMU....
ALAFU MUMFANYIE NA KITU MBAYA MAANA HUYU NAHISI ANASUMBULIWA NA NYEGE TU....HIKI KIHEREHERE ALICHONACHO NI NYEGE ZINAMSUMBUA...ANACHOKITAFUTA ATAKIPATA VERY SOON...." 

Machangu wajiuza karibu na nyumba ya Waziri Mkuu







--> KWELI ni aibu kwa taifa kama la Tanzania, lenye ulinzi uliotimia lakini ni ajabu sana kuwaona wanawake wanaoishi mjini kwa kutegemea biashara haramu ya kuuza miili ‘machangudoa’ wamefikia kuifanya jirani kabisa na makazi ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Mizengo Pinda.

WANASWA NA MAPAPARAZI
Wiki iliyopita, mapaparazi wetu  waliwanasa machangudoa hao wakiwa wanazurura kwenye Barabara ya Kenyatta inayopita mbele ya makazi ya waziri mkuu takriban mita 80 kutoka barabarani kwa lengo la kujiuza.
Ili kulijua hilo kwa undani, mapaparazi wetu walijifanya wateja kabla ya kuwapiga picha ili kuweza kuzungumza nao mawili matatu kuhusu kuwepo eneo hilo lenye heshima zake.
Mmoja wa ‘wauza sukari’ hao aliyejitambulisha kwa jina la Hawa, mkazi wa Kinondoni, alikiri yeye na wenzake kufanya biashara hiyo kwenye eneo hilo.
“Ni kweli mimi na wenzangu tunapiga kambi eneo hili, huwa ikifika usiku tunaanzia kule Coco halafu tunakuja hadi huku, lakini mbona maswali mengi, unataka tufanye biashara kama vipi sepa,” alisema changu huyo akianza kupandisha jazba.

WATEJA WAO WAKUBWA NI HAWA
Kikubwa walichokiongea machangu hao walisema barabara hiyo yote hupitwa na viongozi wakubwa na wafanyabishara ambao baadhi yao ni wateja wao wakubwa. Wakasema hawamwamini sana mteja anayekwenda na Bajaj au Bodaboda kwa vile wanasumbua kutafuta eneo la kufanyia ngono.
“Wateja wetu wengi ni wale tunaomalizana ndani ya gari, hawa wa Bajaj na Bodaboda wengi wanataka kwenye majani, ni rahisi kukamatwa na polisi wa doria,” alisema changudoa mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Suzy lakini hakuwa tayari kutaja yaliko makazi yake.

CHAKUJIULIZA SASA
Inakuwaje wauza miili hao watanue eneo ambalo kimazingira linapitiwa na viongozi mbalimbali wazito kama vile mabalozi wa nje waliopo Tanzania, mawaziri, akiwemo waziri mkuu mwenyewe ambaye ni jirani kabisa na makazi yake?

ASKARI WAPO WAPI?
Yapo madai kwamba, askari wanaovalia mavazi ya kiraia ambao wanapaswa kuhakikisha usalama wa eneo lote la Coco Beach wanakaushia matendo hayo kwa kile kinachodaiwa wanapozwa na kitu kidogo.
“Askari wapo, lakini sema baadhi yao wanatufahamu, kwa hiyo ikitokea na sisi mambo yetu yamekaa vizuri tunachekiana,” alisema Suzy.


Source:gpl

Mwanafunzi UDSM ajinyonga hadi kufa

Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mwaka wa pili Kitivo cha Sheria, Joseph Bernadina (25), amejinyonga kwa kutumia kamba na kukutwa ameifunga juu ya mti, katika eneo la Yombo chuoni hapo.

Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Utawala, Profesa Yunus Mgaya, alithibitisha  kutokea kwa tukio hilo na kwamba alipata taarifa hizo jana asubuhi.

Aliongeza kuwa Jumamosi iliyopita alipokea simu kutoka kituo cha polisi cha chuo hicho akielezwa kuwa kuna mwanafunzi alitishia kujiua, lakini aliwahishwa hospitali na kupatiwa ushauri kutoka kitengo maalum cha washauri wa chuoni hapo na kuruhusiwa Jumapili.

“Nilikuja tena kushituka leo asubuhi napokea simu kutoka kwa mshauri wa wanafunzi kuwa kuna wanausalama wamemkuta mwanafunzi akiwa amejinyonga juu ya mti huku akiwa na karatasi kwenye mfuko wa sharti ikimtambulisha pamoja na ujumbe uliosema, kifo chake kisihusishwe na mtu yeyote kwani amejiua kwa ridhaa yake --asisumbuliwe mtu yeyote kwani nimefanya hivi kwa maamuzi yangu mwenyewe pia nizikwe kwetu--” alisema.

Profesa Mgaya alisema taratibu za mazishi zinaendelea kufanywa na Uongozi wa chuo kwa kushirikiana na ndugu wa marehemu na kwamba Chuo kitagharamia kuusafirisha mwili kama alivyoomba katika ujumbe aliouacha wa kupelekwa wilayani Ludewa Mkoa wa Iringa.

Msanii Maringo Saba Anywa Sumu!!

--> Msanii wa vichekesho vya "Mizengwe" kupitia kituo cha ITV amelazwa katika hospitali ya Mwananyamala baada ya kunywa sumu akiwa na nia ya kujia baada ya kumfumania mkewe akivinjari na rafiki yake wa karibu. Udaku unaelezwa kuwa maringo aliwawekea mtego siku nyingi nz arobaini yao ilikuwa imefika wiki iliyopita ambapo baada ya tukio la kuwafumania na mkewe kuamua kula kona jamaa akaona bora ajiue.

Dereva Aliyemgonga Askari na Kumuua Papo Hapo Kortini

DEREVA anayetuhumiwa kwa kesi ya kusababisha kifo cha askari wa usalama barabarani, Koplo Elikiza Nnko, Jackson Steven Simbo (pichani) amefikishwa mahakama ya Kinondoni, Dar, Machi 26,  mwaka huu na kuzua jambo kortini.
Mtuhumiwa huyo baada ya kupata dhamana alikwenda ofisini kwa maofisa wa mahakama hiyo na kubadili shati kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kuondoa nuksi ya kulala rumande kwa siku 8.
Jackson anakabiliwa na makosa matatu,   kusababisha kifo cha Koplo Elikiza, kuendesha gari kwa mwendo kasi na kuingilia msafara wa kiongozi na kushindwa kujisalimisha polisi hadi alipokamatwa. Kesi hiyo itatajwa tena Aprili 15, mwaka huu.

Source:gpl

Monday, March 25, 2013

Eti Isha Mashauzi anatumia Madawa ya Kulevya!



-->




Hatimaye mamaa Isha Mashauzi, mkurugenzi wa bendi ya mashauzi classic amefunguka na kukanusha ya kwamba anavuta bangi, badala yake amesema ya kuwa hupata faraja toka kwa vinyaji vikali na mirungi hasa akiwa anataka kupanda stejini, na kwa vile hana mume wala mtoto basi hizo ndo kampani zake kwa sasa.

Milioni 13 za Wema Sepetu zamrudisha Kajala Uraiani.


-->


Msanii wa filamu za kitanzania Kajala Masanja ameachiwa huru leo mchana baada ya Msanii mwenzie WemaSepetu, kumlipia Faini ya Shilingi Milioni 13 na kumfanya asiende kutumikia kifungo cha miaka mitano jela. Kajala ambaye alihukumiwa akiwa na mumewe ambaye yeye ameenda kutumikia kifungo cha miaka saba jela kutokana na kupatikana na hatia ya kesi iliyokuwa ikiwakabili ya utengenezaji wa fedha haramu. Katika mahojiano na kituo kimoja cha radio nchini, Wema amesema kwamba anajisikia kama shujaa fulani kwa msaidia rafiki yake huyo na ilimchukua kama masaa mawili hivi kumaliza kila kitu.

Sunday, March 24, 2013

Chinua Achebe Afariki Dunia

Profesa Mahiri na mtunzi wa kitabu cha "Things Fall Apart" Chinua Achebe amefariki dunia. Mwandishi huyo maarufu toka Afrika Magharibi amefariki nchini Marekani alipokuwa akiishi baada ya kuugua kwa muda kidogo. Mpaka umauti unamfikia alikuwa akifundisha masomo ya Lugha katika chuo cha Brown, amefarikia akiwa na umri wa miaka 82.

Kuna Ulazima wa Tatoo Mpaka......

-->


Siku za hivi karibuni kumekewa na wimbi la vijana wengi kujipiga tatoo sehemu mbali mbali za miili yao. miongoni mwa sababu zikiwa ni hamasa ya ushabiki au mapenzi yao juu ya kitu fulani au mchezo fulani. Cha kushangaza sasa hali imekuwa too much kiasi kwamba watu wanajipiga tatoo hadi sehemu za siri.

2face Aoa Dubai Jana

Mwanamuziki 2face kutoka nchini Nigeria jana Jumamosi ya Tarehe 23/03 ameuaga U single boy baada ya kufunga pingu za maisha na mwanadada Annie Macaulay. Katika kuhakikisha Mpango mzima unakwenda vizuri, Milionea wa Kinageria ambaye anaishi Marekani Ayri Emami, amechangia Shilingi milioni 20 za Nigeria.

Miss Israel "MWEUSI" Wa Kwanza

-->
Mwanadada Yityish Aynaw, ni mkimbizi toka nchini Ethiopia. Ameweka Rekodi ya kipee pale alipotoa Taji hilio la Mlimbende wa mwaka wa Nchi hiyo juku akiwa na asili ya kiafrika. Inasemekana kuwa mwanadada huyo alihamia nchini humo zamani akiwa bado binti mdogo.

Saturday, March 23, 2013

Kutana na Bingwa wa kujipinda

--> Kwa jina anaitwa Alesha Dixon, akiwa katika moja ya shows zake huko Uingereza, akijipinda zaid ya mpira.

Mvuto wa Kim baada ya Kujifungua


-->















 Picha hiyo ikimwonesha mwanadada Kim Kardashian na Ddada wakiwa matembezini huku akiwa na mvuto kama vile hajajifungua siku za hivi karibuni.

Wednesday, March 13, 2013

Mpango mzima ndani ya Dar Live

-->
Hatimaye magwiji wa hip hop ndani ya wilaya ya Temeke, Dar na Tanzania kwa ujumla, nazungumzia makundi ya wanamuziki ya TMK Halisi na TMK Family yanatarajia kufanya makamuzi ya kufa mtu ndani ya Ukumbi wa Dar siku ya Tarehe 31/03/2013...... Nisikumalizie uhondo.....

Friday, March 1, 2013

Timbulo na Skendo ya Madawa ya Kulevya

< div class="separator" style="border-bottom: medium none; border-left: medium none; border-right: medium none; border-top: medium none; clear: both; text-align: center;">

Habari ambazo bado hazijathibitishwa zinaeleza ya kuwa Msanii Ali Timbulo, maarufu kama Timbulo amekamatwa akiwa na mzigo wa madawa ya kulevya Nchini Burundi, Timbulo ambaye alikwenda nchini humo kupiga show kutokana na maombi ya wapenzi wake wa nchini humo.
Blogger Widgets