Sunday, August 4, 2013

Wanahabari Watatu Wafariki Dunia katika Ajali ya Gari


Umoja wa Wnahabari wa Nigeria (NUJ) Ijumaa hii ulipatwa na pigo kubwa baada ya kuondokewa na wanahabari wake watatu huku wengine zaidi ya Wanne wakijeruhiwa vibaya.

Tukio hilo lilitokea majira ya saa 12 jioni maeneo ya Ilesa, Jimbo la Osun wakati wanahabaro hao walipokuwa wakirudi kutoka katika mkutano Huko Abuja. Mmoja wa majeruhi Bw. Gbenga Opadotun amesema sababu ya kupata ajali hiyo ni mwendo kasi wa gari na kisha Tairi la Mbele Likapasuka.

Baada ya kupasuka kwa tairi la mbele, geri hilo lilipinduka zaidi ya mara nne na kusimamia katika Pori ambapo baadhi ya waliofariki walirushwa hadi nje ya gari kutokana na kutofunga Mikanda.

No comments:

Post a Comment

Blogger Widgets