
Friday, August 21, 2015
Uongozi wa Azam FC umesema hauna tatizo na uamuzi wa Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF) kumbadilisha mwamuzi wa mchezaji wa Ngao ya Jamii,
Jumamosi. Mchezo huo unawakutanisha Azam FC dhidi ya Yanga ambao
utarushwa moja kwa moja na runinga ya Azam TV, sasa utachezeshwa na
Martin Saanya. TFF imembadilisha Israel Nkongo ambaye ameelezwa kuwa na
matatizo ya misuli. Katibu wa Azam FC, Idrissa Nassor amesema wao
wanachotaka ni uchezeshaji wa kufuata sheria 17 za soka. “Kwa kweli
hatuna tatizo, kama sheria 17 za soka zitafuatwa sisi hatuna tatizo.
“Hiyo si kazi yetu, kikubwa ni maandalizi ambayo tumekuwa tukiendelea
kuyafanya,”

Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment